Monday, June 2, 2014

HAZINA YA MAARIFA NA FRED MSUNGU.

By Jimmy  |  10:15 AM No comments


 HITMISHO LA MSIMU WA KWANZA KATIKA HAZINA YA   MAARIFA
                                                    (BADILI CHANZO CHA TAARIFA)                                            

Rafiki msomaji wa safu hii ya hazina ya maarifa ni heshima yangu kubwa sana kukushukuru kwa kunipa nafasi  na muda wako ili nikuhudumie kwa njia ya maandishi.Imekua safari ndefu ya majuma kadhaa ambapo kwa pamoja tulipata wasaa wa kujifunza juu ya taarifa na namna jinsi ambavyo taarifa inaweza kua ni chanzo cha matokeo fulani katika maisha yako.Tumejifunza na kuangalia mambo mengi sana hasa kuhusiana na vyanzo mbali mbali vya taaarifa jinsi vilivyo na uwezo mkubwa wa kubadili maamuzi yako na tuliona kwamba maamuzi huleta hatua ya matendo na tendo ndilo huleta matokeo.Sasa watu wengi tumekua tukishugulika sana na matokeo na kusahau kwamba mzizi wa tatizo au mafanikio si matokeo bali ni ile taarifa ulioipokea na kuiamini.Hivyo aina ya taarifa unayoipokea itaamua sana aina ya hatma yako pia,Ninaamini kwa namna moja au nyingine safu hii imekua msaada mkubwa wa kupindua fikra yako na kukupa uwezowa kuwaza kwa namna nyingine na kuliendeleza wzo kua endelevu ili uendelee kupata matokeo mapya.

MUHIMU                                                                                        
Haijalishi ni taarifa ngapi potofu ulizozipata mpaka sasa,na hii inaweza kua kwa kujua au kwa kutokujua.Kitu unachotakiwa kutambua kua jana imepita na haitarudi tena milele yako yote..yaliyotokea jana huwezi kuyabadili yatabaki kua historia.Lakini habari njema hapa ni kwamba una maamuzi makubwa sana juu ya kesho yako,Haijalishi umeharibu kwa kiasi gani katika maisha yako na haijalishi umesikia nini na umefeli mara ngapi kwa ukosefu wa taarifa sahihi!JANA IMEPITA LAKINI KESHO IKO MIKONONI MWAKO....Leo ni siku mpya ya kipekee ambayo ukizingatia maneno haya ambayo pengine unaweza kuyasoma na kuona ni ya kawaida sana lakinii nakwambia kwamba ni sekunde moja tu ya utii wa neno inatosha kubadili historia yako.Bado unanafasi ya kuibadili kesho yako kua ni ya mafanikio ambayo kwa hakika kama utaamua kufanya hivyo itabadili mtazamo wako na kukufuta machozi yako ya jana pale ulipoanguka na kushindwa.BADILI CHANZO CHA TAARIFA UPATE MATOKEO MAPYA.
 HITIMISHO/SHUKRANI
Leo ndio J3 ya mwisho kabisa katika safu yetu hii ya hazina ya maarifa msimu wa kwanza ambao tulikua tukijifunza kwa pamoja kitu kiitwacho....BADILI CHANZO CHA TAARIFA.Haimaanishi kwamba leo ni mwisho wa safu hii hapana lakini kwa msaada wa Mungu ninaamini katika msimu wa pili wa safu hii kuna mambo mazuri na makubwa zaidi ambayo yanakuja kwajili yako rafiki yangu msomaji unaezifuatilia safu zangu kupitia mtandao huu.

  SHUKRANI 
Namshukuru sana Mungu ambae yeye ni nafasi ya kwanza kwangu kwa kunipa kipaji uwezo na kibali cha kuifanya kazi hii,Lakini pia nawashukuru sana wasomaji wangu wote kwa kua bega kwa began a mimi katika safari hii.Pia kipekee sana nimshukuru rafiki yangu Jimy temuu ambae ndie mmiliki wa bolg kwa kulipokea wazo langu na kuniamini kunipa umanja wa kuweza kuandika katika ukuta huu.Pia marafiki zangu wengine wengi ambao tumekua bega kwa bega kuufanikisha mzigo huu kwenda hewani...James Kalekwa(PHD) Samuel sasali Prosper Mwakitalima na kipekee zaidi wewe unasoma hivi sasa.
Unataka kujua msimu wa pili katika safu hii kunani....? Basi tukutane kupitia ukuta huu huu siku ile ile...........kaa tayari
KWA MAONI NA USHAURI
Fredymsungu@gmail.com
0653 318117
0798 020103
FACEBOOK ACCOUNT     FRED MSUNGU
WHATSAPP   0653 318117
Mungu akubariki sana .........
WAPINDUA ULIMWENGU (MAPINDUZI YA FIKRA)

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP