Thursday, April 17, 2014

MAKUTANO YA TAI na JAMES KALEKWA

By Jimmy  |  10:10 AM 1 comment


PASAKA WA PILI NI UREJESHO WA KUSUDI KUU LA KWANZA LA UFALME WA MUNGU.


Utangulizi

“Sikukuu” ya Pasaka inatokana (asili yake) na maandiko ya neno la Mungu yaani Biblia (Rejea kitabu cha Kutoka 12:1-51). Humo ndimo unapatikana mwanzo wa habari ya Pasaka na namna inavyopaswa kuwa. Hata hivyo mtazamo wa watu wengi na dunia kwa ujumla juu ya Pasaka umebadilika sana. Wengi wameichukulia kuwa kama siku, wengine huitambua kama siku na hata baddhi ya watu huiona kama maadhimisho tu na hivyo kuifananisha na siku, Sikukuu au maadhimisho mengine ya kawaida kabisa. Jambo la msingi ninalotamani sana ujifunze katika safu hii ya makutano ya tai ni kwamba Pasaka ni sadaka wala si siku/Sikukuu/maadhimisho. Jambo jingine ni kwamba, Pasaka kama sadaka haikutolewa kwa bahati mbaya bali kulikuwa na kusudi la kutolewa kwa dhabihu hiyo
Ufalme wa Mungu ni kusudi kuu la uumbaji wa Mungu tangu milele. Mafundisho juu ya ufalme wa Mungu yamekuwa yakitolewa kwa uchache sana ndani ya kanisa la zama zetu. Hivyo katika mafundisho haya nitaonyesha jinsi gani Yesu Kristo ambaye ndiye Pasaka wa pili (1Wakorintho 5:7-8) alikufa ili kurejesha kusudi kuu la awali la Mungu kwa habari ya
mwendelezo (extension) wa ufalme wake katikati ya wanadamu (Wakolosai 1:13).

Fuatana nami katika mafundisho haya na maisha yako hayatakuwa kama yalivyo!

 Kutoka 12:1-51
Taifa teule la Mungu, Israeli walikaa katika hali ya utumwa chini ya ufalme mwingine (bila kuwa na uongozi wa Mungu) kwa miaka 430 (Rejea Kutoka 12:40b).
Kuwa mtumwa maana yake kuishi chini au/na kwa utashi wa bwana mwingine (si kama utakavyo). Na kuwa chini ya ufalme (wa Mungu ama wa ulimwengu) ni kuishi matakwa/mapenzi ya mfalme aongozaye. Sasa, wana wa Israeli walikuwa chini ya ufalme, si ufalme wa Mungu, bali ufalme wa Misri uliokuwa ukiongozwa na Farao (mfalme wa Misri). Maana yake ni kwamba waliishi mapenzi/matakwa ya mfalme asiye mfalme wao… Kwa lugha nyepesi sana na ya kueleweka, walikuwa ni mateka (captives).
Waisraeli walitumikishwa na kufanya kazi ngumu na nzito (Kutoka 1:13-14); watoto wao wa kiume waliuwawa (Kutoka 1:16). Kazi ngumu na nzito walizofanya zinathibishwa na moja ya maajabu saba ya dunia, yale mapiramidi (pyramids) ya Misri… Hakuna mashine au mitambo inayoweza kufanya kazi kubwa kiasi kile – ndiyo maana mapiramidi ni maajabu ya dunia! Waisraeli hawakuyafurahia maisha wala kuufurahia uumbaji wa Mungu kwasababu walikuwa katika hali ya utumwa na chini ya ufalme.
Waliozaliwa na kuikuta hali hiyo, walichukulia kuwa ndiyo kawaida ya maisha kwasababu hawakuwahi kuijua kawaida nyingine… Utumwa na kuwa chini ya utawala ukawa ni uzoefu wa maisha yao kila siku (daily experience). Akili yao ikafungwa na mfumo wa maisha yao ya kila siku hii ikawapelekea kujenga fikra za kitumwa (slavery mindset/mentality). Walijichukulia kuwa wao ni wa hivi hivi, lasivyo angepatikana mmoja kati yao ambaye angewaza tofauti na kutafuta suluhu ya matatizo yao. Akili zao hazikuweza kufikiri maisha nje ya utumwa na ufalme wa Misri (They couldn’t comprehend what it feels/means out of bondage and out of Pharaoh’s kingdom)… Hebu nikuonyeshe jambo muhimu sana hapa, usiruhusu mazingira yako kukuaminisha ya kwamba huwezi kutoka kwenye hayo! Unaweza kuwa zaidi ya mazingira yanavyosema, unaweza kuwa zaidi ya hali zinazokuzunguka… Mtanzania umesikia mara nyingi tukiitwa, nchi maskini, nchi zenye kipato kidog, nchi changa n.k nakuambia katika ujasiri wa Yesu Kristo unaweza kuwa zaidi ya hapo!
Mateso ya utumuwa yalikuwa makubwa na makali kiasi kwamba wana wa Israeli hawakujua wafanye nini zaidi ya kulia kilio kikuu. Hakuna kati yao aliyekuwa na jibu la matatizo yao (Kutoka 2:23-25). Hawa ndugu waliona jambo pekee wanaloweza kufanya ili kujinasua kwenye hilo tatizo ni kulia kilio kikuu!!! Ooh, Mungu akusaidie usiwe kama wao… Hakuna aliyesimama na kuwahamasisha, hakuna aliyekataa hali hiyo, hakuna aliyewaza mawazo mbadala, hakuna aliyejitutumua na kujipiga kifua ili kuleta upinzani kwenye hali yao ya utumwa. Wanaume walilia na wanawake vivyo hivyo; watoto kwa wazee… Kila mmoja alilia kilio kikuu! Ninachotaka uone hapa ni kwamba, kulia hakusaidii jambo lolote, kujihurumia au kulalamika hakuondoi hata chembe/nukta ya “utumwa”… Mpaka mtu asimame afanye jambo!
Na baada ya hapo tunaona Mungu anaingilia kati na kuanza mpango wa kuwakomboa wana wa Israeli kutoka katika hali hiyo mbovu. Jambo ambalo moyoni mwangu ninatamani ulione kwa 



Mtayarishaji na mwandishi wa makala haya ni mwanataaluma na mwalimu.
Kwa mawasiliano zaidi:


James Kalekwa
+255 754 917 764
+255 714 762 669
kalekwajames@gmail.com

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

1 comment:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP