Monday, August 20, 2012

WAKALI WANAO KIMBIZA FACEBOOK.

By Jimmy  |  4:31 PM No comments

Kuna watu maarufu hapa mjini lakini kuna maarufu wa Facebook.Unaweza usinielewe katika hili lakini wao chochote wanacho andika katika Walls zao wana watu wengi ambao hupita nakutoa Comments zao.Wapo ambao wakiandika hata ujinga au kichekesho lazima watu watatoa Comments zao.

Leo naomba nikulete baadhi ya watu maarufu katika Facebook ambao hapa mjini wana mashabiki kedekede pale wanapo andika jambo lolote katika Walls zao.Kama kuna wengine unawajua tafadhari nifahamishe katika kiboksi cha "Lets Chart Here" pembeni mkono mwakushoto wa Blog

WATU 6 MAARUFU KATIKA FACEBOOK

Masanja Mkandamizaji.

Huyu kwangu atakuwa mtu wa kwanza {No1}ambaye yeye huandika vichekesho na vituko. Mara anapo andika upita watu wengi kutoa Comments zao.Kama kuna siku umeamka hauko vizuri na una hitaji kucheka na kupunguza msongo wa mawazo pita kwenye wall yake ufurahi na roho yako.

Mfano wa watu wanao comment kwenye wall yake.

Blogger Sam Sasali

Kijana huyu mtoto wa Pastor yeye huwa hatabiriki hata siku moja.Yeye ukimleta kwenye ishu za Siasa yupo,Vituko yupo vitu siriazi vya maisha ndio usiseme.Na kwa sasa anamtindo wake wa kuanza na maneno ya Tenzi za Rohoni pale kunapokucha asubuhi.Ukiingia tu kwenye Wall yake asubuhi utaona maneno ya nyimbo za Tenzi za Rohoni.Kama huamini pitia wall yake.

Huyu kwangu nampa namba mbili kama mtu anaepata Comments nyingi katika Wall yake.
Rose Mushi.

Dada huyu napenda kumuita mpiganaji na mwanaharakati katika tasnia ya Uwalimu katika kufundisha vijana na hata maswala mbalimbali katika jamii.Ni Dada aliejaliwa busara na hekima katika kupambanua mambo na kwenda na wakati na majira ya sasa.
Nathubutu kusema atakuwa mwana Dada namba moja kwa wadada wanaopata Comments nyingi katika Facebook lakini kwa mimi nampa namba tatu.

Hii ni sehemu ya moja ya jambo alilo andika katika Wall yake kwenye Facebook.

Poul Mashauri.

Kama ni mafanyikio kwa Kaka huyu basi sasa amepiga hatua kubwa,kwa sasa anakampuni kubwa yenye jina la East Africa Bureau Speakers na amekuwa na watu wengi wanaopitia kwenye Wall yake nakuangali nini amesema.Pamoja na ubize aliokuwanao haiwezi kupita siku asiandike jambo lolote katika Wall yake.

Wakati mwingine watu wanaweza wasi Comment lakini waka "like" kile alicho andika.Kwangu nampa namba tano.

Seth Katende.

Kijana huyu yeye anawafuasi wengi wa Dada.Hutumia akili kidogo na watu wengi upita kutoa Comment.Vijana wa kisasa hupenda kumuita Kaka wa malove dav.Hii ni moja kati ya jambo aliloandika kwenye Wall yake siku ya leo.
Kijana huyu nampatia namba tano katika listi yangu.

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP