Monday, April 30, 2012

JENGO JIPYA LA ZINDULIWA KANISA LA KKKT KIJITONYAMA.

By Jimmy  |  10:15 AM No comments


Jengo Jipya la KKKT Kijitonyama.




Dk. Alex Malasusa,Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania akiwa katika ibada ya kuwekwa wakfu jengo la kitega uchumi lililojengwa na kanisa hilo usharika wa Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, jana.Dr Alex alikiri kuchukizwa kwake na baadhi ya makundi yanayotaka kulazimisha mambo ya hovyo yakiwemo ya kishoga kuingizwa katika Katiba.

Mbali na hilo, alikemea vikali tabia zinazofanywa na baadhi ya viongozi walioshindwa kusimamia rasilimali kwa maslahi ya nchi, badala yake wamejimilikisha wao.

Alisema kutokana na ubadhirifu huo, vijana wengi wamekosa ajira na kukiri kuwa ni jambo lililochangiwa na upendeleo katika baadhi ya taasisi.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na viongozi kadhaa akiwemo Waziri Mkuu mstaafu Federick Sumaye, Anna Mkapa pamoja na wengine.

Mbali na jengo hilo lililogharimu sh bilioni 3.5, Malasusa alibariki nyumba iliyonunuliwa na kanisa hilo yenye thamani ya sh milioni 500 kwa ajili ya kuendesha shughuli mahsusi za kanisa.

Source-Sam sasali..







Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP