Monday, May 12, 2014

HAZINA YA MAARIFA NA FRED MSUNGU.

By Jimmy  |  10:36 AM No comments


(FUNZO KUU SIMAMIZI) KIINI CHA SOMO

Hesabu 13:25- 33

Ndugu msomaji wangu tafadhali fuatilia kwa makini safu ya mtiririko wa baada ya kujifunza kwa muda wa majuma kadhaa sasa leo ni fulsa nyingine ya ya kuangalia kiini cha somo kwa mtiririko uliochambuliwa kutoka kwenye vyanzo mbali mbali kama Biblia,vitabu na nyenzo nyinginezo(marudio yenye uchambuzi yakinifu)

Mara nyingi maono/malengo huchukua muda mrefu mpaka kufikia katika hatua ya mchakato wa matendo ambayo yataleta uhalisia wa
kitu husika, Lakini pamoja na matarajio, maono au malengo ya muda mrefu nataka tuone jinsi vile taarifa inavyoweza kubadili kwa haraka muono wako na kile ulichokitarajia. (Matokeo sahii huja kwa chanzo sahihi na taarifa sahihi...Matokeo mabaya huja kwa chanzo kibaya na taarifa mbaya)

Hesabu 13:25- 33

13.25 Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini.

13.26  Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.

13.27  Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake.

13.28  Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko.

13.29  Amaleki anakaa katika nchi ya Negebu; na Mhiti, na Myebusi, na Mwamori wanakaa katika milima, na Mkanaani anakaa karibu na bahari; na kando ya ukingo wa Yordani.

13.30  Kalebu akawatuliza watu mbele ya Musa, akasema, Na tupande mara, tukaitamalaki; maana twaweza kushinda bila shaka.

13.31  Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.

13.32  Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.

13.33  Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.

Hii ni habari ya wana islael ambao walitoka misri kwa lengo/wazo moja la kwenda kanaani kwenye nchi ya ahadi ambayo Mungu aliwaahidi ni habari ndefu lakini lengo au mkazo wa somo letu uko kwenye mistari hiyo michache tuliyosoma hapo juu.Mungu alimwambia musa atume wapelelezi kwenda kuichunguza nchi ile sasa ukisoma hapo juu kuanzia huo mstari wa 25 utaelewa zaidi....

Ukisoma habari hiyo utagundua kutumwa kwa wale wapelelezi lengo  ilikua ni kuleta habari ambayo ingekua msaada kwao ili wajue wanapaswa kuingiaje katika mji ule....Sasa lengo kuu hapa ilikua ni habar,habari ya aina  yoyote ile itakayo wajia iwe nzuri au mbaya,ili kutimiza lengo la kuifikia ile nchi ilikua ni lazima wasonge mbele. Lakini ukisoma kuanzia mstari wa 28 utaona jinsi watoa taarifa (wapelelezi) walivyoanza kubadili mtazamo wa watu kupitia taarifa yao mbaya iliyotokana na uchunguzi walioufanya.Ukiendelea kusoma utaona walizidi kupamba maneno kiasi cha kusababisha umati wote kuamaki na kukubaliana na maneno yao......Rejea mstari wa 31- 33.

Ilifika mahali wakajifaninisha na panzi, na ukiendelea kusoma sura inayofuata utaona jinsi watu walivyoingiwa hofu na kuanza kulalamika ilifika mahali Mungu akaghadhibika na katika umati wote ule wa watu waliokua na ndoto za kuifikia nchi ya kaanani na kuimiliki ni watu wawili tu ndio ambao walifanikiwa kuingia nchi ile. (Hesabu 14:22-24)

MUHIMU:  Ukichukua wasaa na kusoma vizuri juu ya habari hii utatambua kwamba watu hawa si kwamba walikurupuka kuanza safari ile..la hasha! Hii ilikua ni ahadi na mpango kamili kabisa wa Mungu ambayo ulikuwepo toka vizazi na vizazi na waliishi miaka yote wakiisubiri ahadi hiyo.Lakini ghafla baada ya kusubiri ya kuhangaika kwa miaka mingi utaona hapa kuna kitu kinatokea ambacho kinasababisha mambo kuharibika ghafla,Kitu hicho ni TAARIFA.Haijalishi ni kwa muda mrefu kiasi gani umehangaika kufanya kitu au umekua katika mchakato wa kungoja matokeo ya malengo yako,unapoiruhusu tu  taarifa potofu iingie katika ufahamu wako jua wazi inaweza ikaua juhudi na nguvu  yote uliyoitumia na ukapata hasara kwa haraka  ukilinganisha na muda ulioutumia katika mchakato wa kuyatengeneza matokeo(KUBOMOA NI RAHISI KULIKO KUJENGA) Niliongea awali kwamba taarifa ni taarifa tu haijalishi kwamba ni nzuri au mbaya maadam ni taarifa lazima itaathiri maamuzi na matokeo yako.Pamoja na taarifa mbaya walioipokea watu hawa walikua na uchaguzi wa kufanya kwasababu kuna watu ambao walileta taarifa nzuri lakini waliipuuza na kuchagua kusikiliza na kuiamini taarifa mbaya na potofu ambayo iliwagharimu sana............
Unaweza kuwasiliana na mwandishi kupitia namba 0653-318117, ama kwa barua pepe fredymsungu@gmail.com 

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP