Monday, April 28, 2014

HAZINA YA MAARIFA NA FRED MSUNGU.

By Jimmy  |  7:20 AM No comments

 SAFU YA FRED MSUNGU: BADILI CHANZO CHA TAARIFA
JINSI ULIVYO LEO NI MATOKEO YA ULICHOKISIKIA NA KUKIAMINI

SEHEMU YA NNE.....

       I.            NINI CHANZO SAHIHI NA NINI SI CHANZO SAHIHI CHA TAARIFA
Jibu la swali hili linategemea sana na maisha uliyochagua (hatma yako) na aina ya malengo uliyonayo.Inawezekana sana chanzo hicho hicho kikawa ni sahihi sana kwa wengine  lakini kwako  kisiwe ni sahihi,Naweza nikawa nimekupa wakati mgumu wa kufikiri lakini kadri unavyozidi kusoma ndivyo fikra yako inapanuka na ninaamini mpaka mwisho tutakua kwa pamoja tumeipata maana halisi ya somo hili.
MUHIMU: Jambo la muhimu sana kujua hapa ni hili ‘ Huwezi kuja kuyafikia matokeo makubwa zaidi ya fikra zako zinavyoona....Jinsi vile unawaza ,unaona juu yako na juu ya kesho (hatma)yako ndivyo vile utakavyokua.Hakuna muujiza wala uchawi wa aina yeyote katika hili ,Kipimo au kiwango ulichonacho juu yako ndicho hicho
utakua milele.(Mithali 23:7 )Ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo.
Ukiisoma hiyo mithali utaona hapo ametumia neno ‘Ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo’ Naliangalia kwa jicho la tofauti sana neno NDIVYO ALIVYO!Maana ninayoipata hapa ni kwamba kile unachokiona ndani yako haijalishi kimekwisha kutokea (kudhihirika)au bado hakijatokea lakini vile unaona ndivyo ulivyo.Maana yake hapa kama unaona ukuu ndani yako tayari wewe ni mkuu ila kuna hatua ambayo unatakiwa kuifanya tu ili kudhihirisha ile hali ilio ndani yako iwe katika ulimwengu halisia.Moja kati ya hivyo kupata chanzo sahihi kitakacho kuwezesha kuthibitisha hali yako ya ndani nje.Pia kama unaona madhaifu ndani yako maana yake hivyo ndivyo ulivyo kwasababu hicho ndicho unachoona.Mtu alie na ukuu ndani yake ana kazi ya kuuthibitisha maana matokeo ya ukuu hayawezi kuonekana wala kufaidia kitu mpaka yamethibitika kwa watu wengine.Lakini mtu unaeona mapungufu(mpumbavu) ndani yake wala hana kazi yeyote ya kukuthibitishia maana utamuona tu jinsi anavyoishi,anavyo waza na hata usemi wake tu utamuelewa huyo ni mtu wa namna gani.



UMESIKIA NINI....TOKA KWA NANI?
Chanzo cha taarifa mara nyingi ndio hua chanzo cha kuakisi na kukuaminisha kitu fulani ambacho baada ya kukisikia, kuona au kusoma na kukiamini na kuiweka imani katika matendo baada ya muda fulani wa mchakato matokeo huja vile vile kama jinsi uliona au kuamini.
Inawezekana wewe ulianza kuuona ukuu ndani yako....katika biashara, huduma, masomo, siasa au uongozi, Sasa baada ya kuhisi kitu hicho ndani yako ni taarifa gani ulioipata juu yako au juu ya ndoto yako? Je chanzo cha hiyo taarifa yako kilikua sahihi?  Ukijizoesha kusikia habari za kushindwa basi unajijengea matokeo ya kushindwa kwasababu ubongo wako umekaa tayari kupokea taarifa, kufikiri na kuifanya fikra kua imani na imani kua katika matendo na kuleta matokeo halisi na kama kushindwa ndio imekua taarifa yako basi jiandae kushindwa.


Kama jinsi ulivyoona huo mtirirko katika kifani chetu hapo juu hivyo ndivyo taarifa husafiri na mwisho wake hua ni matokeo ambayo yanaweza kua mazuri au mabaya, lakini inategemea sana pale mwanzoni ulianza kwa kupokea taarifa gani! Kama taarifa ilikua ni sahihi basi tegemea matokeo sahihi ya yenye manufaa, Lakini kama haikua sahihi basi tegemea matokeo yasio sahihi pia.Somo hili litaendea J/tatu ijayo,usikose kuendelea kufatilia safu hii iliyoandaliwa na Fred Msungu.Kwa mawasiliano zaidi piga simu No 0653-318117 au fredymsungu@gmail.com.

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP