Monday, April 21, 2014

HAZINA YA MAARIFA NA FRED MSUNGU.

By Jimmy  |  6:26 AM No comments

 SAFU YA FRED MSUNGU: BADILI CHANZO CHA TAARIFA
JINSI ULIVYO LEO NI MATOKEO YA ULICHOKISIKIA NA KUKIAMINI

SEHEMU YA TATU.....


FIKRA TATA: 2
Siku za hivi karibuni kuna uvumi umechukua umaarufu sana kwenye akili za watu na kwenye vichwa mbalimbali vya habari  juu ya watu wenye mafanikio makubwa.Imani za watu wengi sasa zimejengeka kwamba haiwezekani mtu kufanya kazi au kua na bidii katika eneno lake na akafanikiwa bila viambatanishi vya ziada,Hivyo uchawi umevuma sana kua  ni chanzo cha mafanikio kwa watu wengi.Wengine wamekwenda mbali zaidi na kuanza kuongea habari za freemason na kuwahusisha watu kadhaa waliofanikiwa  na tuhumma hizo,Hii imechangia sana kupunguza mori na ufanisi wa watu katika utendaji wakiamini kwamba ukitaka mafanikio haiwezekani bila kujiambatanisha na hivyo vitu.Binafsi niko kinyume sana na dhana hiyo,sipingi kwamba uchawi upo na kwamba kuna watu wanaofanikiwa kwa njia zisizo halali...la hasha! lakini ninachopinga hapa ni watu kujipa dharula na kupunguza ufanisi na kukaa chini kuwaza kwamba watu wengi wenye mafanikio wanajihusihsa na mambo haramu
kama hayo.Kwa mtazamo wangu kama wewe ni mtu wa maono na ndoto kubwa  katika maisha yako  kuhusisha mafanikio ya mtu na uchawi,freemason au nguvu nyingine ya ziada sidhani kama hicho ni chanzo kizuri cha taarifa kwako.Mtu yeyote mwenye ndoto au matarajio makubwa mara zote huwaza chanya na sio hasi.Maana kama haiwezekani kufanikiwa bila kujihusisha na vitu hivyo basi inamaanisha na wewe hautaweza kufikia malengo yako .Mtu mkuu huwaza mambo makuu ndani yake na mambo makuu ni yale tu yanayotokana na fikra sahihi (chanya)  Hivyo ushauri wangu kwako ukiwa na ndoto za ukuu ndani yako achana na mawazo ya watu wanaovumisha mambo yasio na manufaa,Ongeza juhudi, maarifa,kaa kwenye lengo na pokea taarifa sahihi kutoka kwenye chanzo sahihi utapata matokeo sahihi.

(Hagai 2:8) Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu asema bwana wa majeshi.  Andiko hili linabeba maana nzima ya mafanikio japo hapo ameongelea kuhusu fedha na dhahabu,Sasa kama fedha nadhahabu ni mali ya baba yako maana halisi hapa ni kwambaunanafasi ya urithi katika vitu hivyo.Ni swala la kujitambua tu na kuchukua hatua ya kufanya wajibu wako ili upate haki yako. HAKUNA HAKI BILA WAJIBU...Hii ina maana kuna mambo ambayo ni lazima uyafanye kwanza ili kwayo upate kumiliki.
       I.            NINI CHANZO SAHIHI NA NINI SI CHANZO SAHIHI CHA TAARIFA
Jibu la swali hili linategemea sana na maisha uliyochagua (hatma yako) na aina ya malengo uliyonayo.Inawezekana sana chanzo hicho hicho kikawa ni sahihi sana kwa wengine  lakini kwako  kisiwe ni sahihi,Naweza nikawa nimekupa wakati mgumu wa kufikiri lakini kadri unavyozidi kusoma ndivyo fikra yako inapanuka na ninaamini mpaka mwisho tutakua kwa pamoja tumeipata maana halisi ya somo hili.
MUHIMU: Jambo la muhimu sana kujua hapa ni hili ‘ Huwezi kuja kuyafikia matokeo makubwa zaidi ya fikra zako zinavyoona....Jinsi vile unawaza ,unaona juu yako na juu ya kesho (hatma)yako ndivyo vile utakavyokua.Hakuna muujiza wala uchawi wa aina yeyote katika hili ,Kipimo au kiwango ulichonacho juu yako ndicho hicho utakua milele.(Mithali 23:7 )Ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo.
Ukiisoma hiyo mithali utaona hapo ametumia neno ‘Ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo’ Naliangalia kwa jicho la tofauti sana neno NDIVYO ALIVYO!Maana ninayoipata hapa ni kwamba kile unachokiona ndani yako haijalishi kimekwisha kutokea (kudhihirika)au bado hakijatokea lakini vile unaona ndivyo ulivyo.Maana yake hapa kama unaona ukuu ndani yako tayari wewe ni mkuu ila kuna hatua ambayo unatakiwa kuifanya tu ili kudhihirisha ile hali ilio ndani yako iwe katika ulimwengu halisia.Moja kati ya hivyo kupata chanzo sahihi kitakacho kuwezesha kuthibitisha hali yako ya ndani nje.Pia kama unaona madhaifu ndani yako maana yake hivyo ndivyo ulivyo kwasababu hicho ndicho unachoona.Mtu alie na ukuu ndani yake ana kazi ya kuuthibitisha maana matokeo ya ukuu hayawezi kuonekana wala kufaidia kitu mpaka yamethibitika kwa watu wengine.Lakini mtu unaeona mapungufu(mpumbavu) ndani yake wala hana kazi yeyote ya kukuthibitishia maana utamuona tu jinsi anavyoishi,anavyo waza na hata usemi wake tu utamuelewa huyo ni mtu wa namna gani.

 

FIKRA TATA: 2
Siku za hivi karibuni kuna uvumi umechukua umaarufu sana kwenye akili za watu na kwenye vichwa mbalimbali vya habari  juu ya watu wenye mafanikio makubwa.Imani za watu wengi sasa zimejengeka kwamba haiwezekani mtu kufanya kazi au kua na bidii katika eneno lake na akafanikiwa bila viambatanishi vya ziada,Hivyo uchawi umevuma sana kua  ni chanzo cha mafanikio kwa watu wengi.Wengine wamekwenda mbali zaidi na kuanza kuongea habari za freemason na kuwahusisha watu kadhaa waliofanikiwa  na tuhumma hizo,Hii imechangia sana kupunguza mori na ufanisi wa watu katika utendaji wakiamini kwamba ukitaka mafanikio haiwezekani bila kujiambatanisha na hivyo vitu.Binafsi niko kinyume sana na dhana hiyo,sipingi kwamba uchawi upo na kwamba kuna watu wanaofanikiwa kwa njia zisizo halali...la hasha! lakini ninachopinga hapa ni watu kujipa dharula na kupunguza ufanisi na kukaa chini kuwaza kwamba watu wengi wenye mafanikio wanajihusihsa na mambo haramu kama hayo.Kwa mtazamo wangu kama wewe ni mtu wa maono na ndoto kubwa  katika maisha yako  kuhusisha mafanikio ya mtu na uchawi,freemason au nguvu nyingine ya ziada sidhani kama hicho ni chanzo kizuri cha taarifa kwako.Mtu yeyote mwenye ndoto au matarajio makubwa mara zote huwaza chanya na sio hasi.Maana kama haiwezekani kufanikiwa bila kujihusisha na vitu hivyo basi inamaanisha na wewe hautaweza kufikia malengo yako .Mtu mkuu huwaza mambo makuu ndani yake na mambo makuu ni yale tu yanayotokana na fikra sahihi (chanya)  Hivyo ushauri wangu kwako ukiwa na ndoto za ukuu ndani yako achana na mawazo ya watu wanaovumisha mambo yasio na manufaa,Ongeza juhudi, maarifa,kaa kwenye lengo na pokea taarifa sahihi kutoka kwenye chanzo sahihi utapata matokeo sahihi.

(Hagai 2:8) Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu asema bwana wa majeshi.  Andiko hili linabeba maana nzima ya mafanikio japo hapo ameongelea kuhusu fedha na dhahabu,Sasa kama fedha nadhahabu ni mali ya baba yako maana halisi hapa ni kwambaunanafasi ya urithi katika vitu hivyo.Ni swala la kujitambua tu na kuchukua hatua ya kufanya wajibu wako ili upate haki yako. HAKUNA HAKI BILA WAJIBU...Hii ina maana kuna mambo ambayo ni lazima uyafanye kwanza ili kwayo upate kumiliki.Somo hili litaendea J/tatu ijayo,usikose kuendelea kufatilia safu hii iliyoandaliwa na Fred Msungu.Kwa mawasiliano zaidi piga simu No 0653-318117 au fredymsungu@gmail.com.



Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP