Saturday, March 29, 2014

KUTOKA NCHI YA CANADA HUYU NDIYE MUIMBAJI WA TANZANIA ANAYEFANYA KWELI.

By Jimmy  |  12:55 PM No comments

Milca kakete
Milca kakete hakumbuki vizuri ni umri gani alioanza nao kuimba maana alikuwa mdogo sana pengine kati ya miaka 5. Aliongoza baadhi ya nyimbo katika kwaya iliyojulikana miaka ya nyuma Tabora ambapo wimbo kama “yuko wapi aliyezaliwa” wengi wanajua wimbo ila hawajui ni Milca aliyeimbisha wimbo ule...Utukufu kwa Mungu.
 
 Mnamo mwaka 1999 na 2000 akiwa kiongozi wa sifa katika Kanisa la Pentecoste Kurasini alipelekwa na Kanisa kuhudhuria semina ya viongozi wa sifa nchini Kenya.Mwaka 2003 akiwa amehamia mjini Arusha,Mungu akaongea naye kutoa album ya kuabudu inayokwenda kwa jina la “Yesu niko mbele zako” na nyimbo nyingine ambazo zilipendwa  kama “Natamani kufanana nawe” “Nifinyange” na “Heri ni jina”

Kwa sasa Milca makazi yake ni Canada ambako bado anafanya
muziki wa injili kama kawaida na kupitia kituo cha VOA Sauti ya amerika
 aliweza kuachia wimbo wake mpya (NAKUNG’ANG’ANIA) ambao unatangaza album yake mpya ya (Video) inayotarajiwa kutoka hivi punde siku za usoni.....unataka kujua mengi kuhusu mwana Dada Milca Kakete endelea kufatilia Unclejimmytemu.blogspot.com kwa habari kamili za Milca.Kwa hisani ya Uncle Jimmy nakupa nafasi ya kusikiliza wimbo wake “Nakung’ang’ania” hapo chini
 

Picha zote kwa hisani ya Milca Kakete

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP