Ni mara chache sana waimbaji wa muziki wa Injili wanapomaliza kufanya tamasha ama event fulani kuwashukuru watu walowapa support kwa namna moja ama nyingine. Katika kazi yangu ya muziki wa injili kwa mara ya kwanza mwimbaji wa muziki wa injili Neema Gasper amenipa nafasi ya kumkumbuka 2013 kwa kuwa ameonesha umuhimu wa kuvishukuru vyombo vya habari viliovyotoa mchango katika kutangaza uzinduzi wake.
Leo majira ya mchana katika Hotel ya Atriums iliyopo Sinza Africa Sana, Neema Gasper ameita watangazaji wa radio za Kikristo na Christian Bloggers pamoja na wadau wa muziki wa injili na kuwashukuru kwa kazi nzuri waliyoifanya katika uzinduzi wa album yake mpya. Baadhi ya vyombo hivyo vya habari ni pamoja na Praise Power Radio, Wapo Radio, Upendo Radio, Christian Bloggers na Clouds TV kupitia kipindi chake cha Chomoza.
Leo majira ya mchana katika Hotel ya Atriums iliyopo Sinza Africa Sana, Neema Gasper ameita watangazaji wa radio za Kikristo na Christian Bloggers pamoja na wadau wa muziki wa injili na kuwashukuru kwa kazi nzuri waliyoifanya katika uzinduzi wa album yake mpya. Baadhi ya vyombo hivyo vya habari ni pamoja na Praise Power Radio, Wapo Radio, Upendo Radio, Christian Bloggers na Clouds TV kupitia kipindi chake cha Chomoza.
Yafuatayo ni matukio katika picha kuhusiana na kilichojiri.
Neema Gasper akishangaa!
Bloggers Samuel Sasali,James Temu,Mwemezi Kyaruzi.
Vero pamoja na Kisaka kutoka Praise power Radio wakiteta jambo.
Peter akiwa busy na msosi hapana chezeaa chakula kwa mwanaume
Ukipata baati ya kukaa na Kisaka hutaboreka mdau wangu.Kitu cha samaki kikishuka mdomoni
Big Boss George Mpela kutoka Praise power sijui chakula kilimshinda.Mana mwili huoo!!
0 comments: