Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri ushirika wa Segerea limenusurika kuteketea kwa moto baada ya
watu wasiojulikana kutupa chupa iliyodhaniwa kuwa na mafuta ya taa au ya
petroli na kulipuka ndani ya kanisa na kuunguza baadhi ya vitu
vilivyowemo katika madhabahu ya kanisa pamoja na gari lililokuwa nje ya
kanisa hilo majira ya saa 8 usiku usiku wa kuamkia leo.
Akielezea tukio hilo
mchungaji wa kanisa la KKKT usharika wa Segerea Bwana Noaha Kipingu,
amesema limetokea majira ya saa 8 za usiku wa kuamkia leo ,wakati
baadhi ya waumini wakiwa ndani ya kanisa katika maombezi ya yaliyoanza
saa 4 usiku kwa ajili ya mkutano unaotarajiwa kufanyika jumapili ya
agosti 25 mwaka huu.
Baadhi ya waumini
walionusurika katika tukio hilo wamesema wamesikia mshindo mkubwa wa
kitu kinachofanana na bomu katika madhabau ya kanisa hilo wakati wakiwa
wamesimama mbele ua kanisa hilo na kisha moto ukaanza kuunguza madhabau
hali iliyowafanya kukimbia na kisha kurudi ndani kwa ajili ya kuzima
moto huo.
0 comments: