Monday, August 12, 2013

CLOUDS FM KUPITIA KIPINDI CHA DINA MARIOS LEO TENA KILIMTEMBELEA MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI SIFA MWENYE KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA NA WASIO JIWEZA.

By Jimmy  |  9:44 AM No comments

Kituo hiki kiko Bunju mwisho kinachoangaliwa na Dada Sifa.Dina aliweza kukijua baada ya kupigiwa simu na mwanamuziki Stara Thomas.Stara alimpigia simu na kumuunganisha na dada Sifa ili aweze kufika katika kitu hicho.
Ana watoto 20 wanao lala na wengine 30 wanaokuja na kuondoka.Hao 30 ni wale ambao wanakaa kwa mama au bibi,babu ila mazingira magumu hawaendi shule wala kupata mahitaji muhimu.Wanakuja kushinda hapo kuna walimu wanafundishwa,wanakula na kushinda na hao wengine jioni wanarudi makwao.
Hapo watoto wanapokaa ni kwa mama yake na Sifa sio kituo rasmi ila Mungu akimjaalia atanunua kiwanja na kujenge nyumba ambayo watoto wanaweza kukaa vyema.Mama yake Sifa ndio anamsaidia kwa kiasi kikubwa kulea watoto wakati yeye akiwa kwenye pilika pilika za huduma ya mziki wa injili







Msaada mkubwa Sifa anaouhitaji kwa watoto wake ni chakula,mavazi,viatu,vifaa vya shule,sabuni za kufua na kuoga,dawa za meno,mafuta ya kupikia na kujipaka.
Pia ikiwezekana apate ml 4 za kununua kiwanja atakachoweza kujenga hapo baadae eneo litakalokidhi mahitaji ya watoto kuishi na kucheza vizuri.
 
Picha wa hisani ya Dina Marios.

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP