Sunday, November 4, 2012

KANISA NCHINI KENYA LASHAMBULIWA....

By Jimmy  |  11:29 PM No comments

Polisi nchini Kenya wanasema watu kama 7 wamejeruhiwa kwenye shambulio la guruneti dhidi ya kanisa katika mji wa Garissa.
Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya na televisheni ya Kenya, KTN, wanasema idadi ya watu waliojeruhiwa inaweza kuwa kubwa zaidi na baadhi ya majeruhi ni mahatuti.
Afisa mmoja amesema kanisa hilo lilikuwa ndani ya kambi ya polisi na guruneti liling'oa paa wakati wa ibada.
Wengi waliojeruhiwa ni askari polisi.
Mji wa Garissa uko karibu na mpaka wa Somalia.
Mwezi wa Julai watu 15 walikufa katika mashambulio kama hayo dhidi ya makanisa mjini Garissa.

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP