Ongoza kimkakati
Mfano wa lengo ambalo ni SMART: Kuihubiri injili kwa watu 1000 nchini
Tanzania katika wilaya 4 kwa mwaka mmoja.
Je, lengo hilo ni hususani (Specific)? Ndiyo kwasababu limetaja idadi ya
watu,idadi ya wilaya na nchi.
Je, lengo hilo Linapimika
(Measurable)? Ndiyo kwasababu ya idadi, eneo
la kijiografia (mahali) yaani mwisho wa siku unaweza kukaa chini na kuangalia
kama wilaya 4 zimefikiwa na kwa kiasi gani, vilevile kuona kama watu 100
wamefikiwa.
Je, lengo hilo linafikika (Attainable)? Ndiyo, kwa Jiografia ya Tanzania
inawezekana kuzifikia wilaya hizo kwa muda huo. Pia unaweza kupata muda wa
kujiandaa, kifedha, kimaombi, ujumbe kwani mwalimu mzuri ni mwanafunzi wa kudumu,
kwahiyo lazima ujifunze ili ukafundishe.
Je,lengo hilo linauhalisia
(Realistic)? Ndiyo, kwasababu muda unaruhusu kufanya mambo mengine kama
maandalizi ya uwanja/ukumbi wa mikutano, mahali pa kufikia, watu wa
kushirikiana nao (si unajua huwezi kushirikiana na watu wote na kwa
upande mwingine huwezi kushirikiana na kila mtu?) n.k yaani kwa lugha ya
kiingereza wanaita "logistics", pia unaweza kuwa na muda wa kutimiza
wajibu wako mwingine kama baba/mama (mzazi), kama mme/mke, kama mtoto na vitu
vya msingi kama hivyo lakini pia kuna jambo la muhimu ambalo watu wengi
hulipuuzia,lakini ni la muhimu sana...MAPUMZIKO! Mungu baada ya kutenda kazi
siku sita alipumzika! Umuhimu wa kupumzika ni kwamba unaporudi tena kwenye
utekelezaji, unakuja na nguvu mpya "fresh".
Mungu akusaidie kuyaelewa haya na kuyatendea kazi na maisha yako hayatakuwa
kama yalivyo, na hayo ndiyo maombi yangu kwa Mungu kwaajili yako msomaji wangu.
Mifano hai ya watu waliotutangulia.
·
Bwana Yesu
Bwana wetu Yesu Kristo aliacha enzi na
utukufu wake huko mbinguni na kuja duniani kufa badala yetu ili atukomboe
kutoka katika laana ya dhambi.Ukitazama katika upana wa yale aliyoyafanya Yesu
akiwa duniani utaona kuwa jambo jingine alikuja kuweka msingi wa maisha
(kielelezo) ambayo watu wote waliomwamini wanapaswa kuyaishi kwa lugha ya
kiiengereza tungeweza kusema Yesu ni role model wa maisha ya imani hii
tuliyonayo!
Bwana Yesu
hakuishi maisha ya kubahatisha, bali alikuwa na malengo; hebu jiulize nini
kilimfanya aanze huduma akiwa na umri aliokuwa nao (miaka 30) na wala si
vinginevyo? Kwanini alichagua wanafunzi kumi na mbili na si ishirini, watano au
arobaini? Kwanini alikufa wakati huo na si wakati mwingine? (Wakati mwingine
Wayahudi walikuja kumkamata Yesu ili wakamshitaki kisha wamuue lakini mwenyewe
alisema wakati wake haujafika, akapita katikati yao na kuwaacha)
Ukisoma kwa umakini maombi ya Bwana Yesu kwaajili ya kanisa lake katika
Yohana 17:1-26, utaona mambo ya uhakika juu ya vitu alivyokuwa akivifanya
mstari 4, "Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile
uliyonipa niifanye." Bwana Yesu anaupata wapi ujasiri wa kujua kazi
amemaliza wakati alijua wazi kabisa kuwa kuna watu wengi tu walikuwa
hawajaokoka bado? alikuwa hajafika sehemu zingine mbali na Mashariki ya kati (Afrika
alikuwa bado hajafika,Asia,Ulaya n.k), sasa kwa hali ya kawaida Yesu alikuwa
bado hajamaliza kazi lakini malengo yote yanapaswa kuwa na ukomo wa muda. Hapo
baadaye katika sura hii kwa kadri ya neema ya Kristo nitakufundisha mambo
yakuzingatia unapoweka malengo na sifa za malengo mazuri. Nakushauri uzisome
kwa upya tena injili nne kwa lengo la kutazama maisha ya Bwana Yesu na malengo.
·
Mtume Paulo
0 comments: