i. Maisha baada ya kifo
Biblia
kwa namna nyingi sana inatuthibitishia ya kwamba kuna maisha baada ya maisha
haya ya sasa na maisha yajayo baada ya haya ni maisha yaliyo na umilele- yaani
yasiyo na mwisho! Lakini si watu wote tutakuwa na maisha sawasawa katika
ulimwengu wa maisha baada ya kifo, kutakuwa na makundi mawili makubwa: mkono wa
kuume na mkono wa kushoto; kondoo na mbuzi; wema na waovu;
paradiso pamoja na
Mungu au ziwa la moto pamoja na shetani na malaika zake. Maisha ya milele
yatakuwa na pande mbili tu na habari njema ni kwamba pande zote zitakuwa ni za
milele.
Katika
muhula huu wa maisha hakuna muda wa kufanya maamuzi na tena si muhula sahihi
kufanya maamuzi. Pia ni muhimu kutambua ya kwamba muhula huu ni muhula wa
kuvuna kutoka kwenye muhula wa pili wa maisha, kuwajibika juu ya ukataji wa
maneno ulioufanya wakati wote ulipokuwa ndani ya bonde.
Waebrania 9:27
“Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara
moja, na baada ya kufa hukumu.”
Mwandishi
waraka kwa Waebrania analeta picha ya kisheria na kimahakama ya kwamba baada tu
ya kufa ni hukumu. Kwa uelewa wa shughuli za kimahakama lazima ujue ya kwamba
hukumu haitolewi kutokana na matakwa, maoni au fikra za upande mmoja (jaji,
utetezi na mashitaka) bali maamuzi ya mahakama yaani hukumu hutolewa kwa kuakisi
ushahidi uliotolewa mahakamani. Kwa namna nyepesi ya kueleweka ni kwamba jaji
hutumia jumla ya ushahidi kama ukweli (facts) na malighafi ya kufanya maamuzi
ya kimahakama. Kwahiyo, jaji/hakimu hatoi maamuzi yake hewani bali kwenye
maisha ya mshitakiwa husika. Kwa mfano mwepesi ni kwamba hakuna mahakama
duniani inaweza kunihukumu kwa kesi ya uhaini hata kama utolewe ushahidi uliojaa
vitabu vikubwa (volumes of books). Hakuna mahakama inaweza kumuhukumu kifo ndugu
Joshua (nimetumia jina kutolea mfano) hata kama kesi itakuwa na mashahidi
milioni moja. Kwanini? Kwasababu hakuna alama hiyo kwenye maisha yangu; hakuna
mtiririko huo kwenye maisha ya ndugu Joshua. Si kwamba mahakama haina uwezo na
wala si kwamba hakimu/jaji ana mamlaka kidogo, bali ni kwasababu maisha yetu
hayastahili hukumu hiyo. Kitu ninachotaka uone ni kwamba kimsingi anayeamua
mwenendo wa kesi au aina ya hukumu ni muhusika (mshitakiwa) na si mtu mwingine
yeyote.
Hebu
nikuonyeshe mfano wenye maelezo mengi zaidi kutoka kwenye kinywa cha ahukumuye
kwa haki, Yesu Krsito mwenyewe.
Luka 16:
25-26
“Ibrahimu
akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako
katika maisha yako, na Lazaro vivyo hivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo
hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi
kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala
watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.”
Kuielewa vizuri hii habari unaweza kuirejea
kutoka kwenye mstari wa 19 mpaka wa 31. Utaona ya kwamba mistari niliyoiweka
hapo juu ni matokeo baada ya maisha ya Lazaro na tajiri wakiwa duniani. Kosa la
yule ndugu halikuwa utajiri bali ilikuwa ni nia yake atumiapo utajiri ule, “…aliyevaa
nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote
kwa anasa…”. Siku zote za maisha alikuwa na nia ya kufanya anasa-
alivaa na kula kwa anasa! Lakini Lazaro hakuwa na nia ya anasa, kula na kuvaa
kwake kulikuwa ni kukidhi mahitaji muhimu… Nia zao kuelekea chakula na mavazi
zilikuwa ni tofauti, umeona, eeh?
Baada ya kufa ndiyo wanakutana katika maisha ya
milele lakini wakiwa kwenye pande mbili tofauti. Kitu gani kiliamua utofauti
huo? Hakuna sehemu Biblia inatuambia kwamba baada ya kufa walifika mahala pa
njia panda na kupewa nafasi za kuchagua wapi watumie maisha yao ya milele,
hakuna! Maisha yao ya baada ya kifo yaliamuliwa na mfumo wa maisha yao kabla ya
kifo – kuwa kifuani mwa Ibrahimu au kwenye mateso ni uamuzi wao wenyewe (tajiri
na Lazaro) na uamuzi huo hufanyika kwenye maisha kabla ya kifo. Kitu
ninachotaka ujifunze hapa ni kwamba maisha ya baada ya kifo si sehemu ya
kufanya maamuzi wala kujitafutia fursa ya kufanya hivyo! Baada ya kifo ni
hukumu na hukumu hiyo inatokana na vile maisha ya kabla ya kifo yalikuwa.
Casino no deposit bonuses, casino games to play free online
ReplyDeleteThe casino no deposit bonus is one you need to know about before you are playing. It is a air jordan 18 retro men red sale really popular 스포츠토토 사기 벳피스트 way air jordan 18 retro men blue to my site of playing online 슬롯 머신 casinos and is not best air jordan 18 retro men blue only a great