Thursday, May 29, 2014

MAKUTANO YA TAI NA JAMES KALEKWA

By Jimmy  |  11:44 AM No comments

Jifunze kuutumia msimu wa maamuzi unufaike!



i.Maisha baada ya kuzaliwa mpaka kifo

 Japo jamii nyingi huyatazama maisha ya mwanadamu katika hatua tatu: kuzaliwa, kuishi na kufa na kimantiki inaweza kuonekana ni kweli lakini unapaswa kung’amua ya kwamba kuzaliwa ni mlango wa kuingilia (entrance) na kifo ni mlango wa kutokea (exit) kwenye jengo fulani. Katikati ya hii miimo miwili ya kimaisha kuna wakati mkubwa wa maisha ambao ni vyema tukaelekeza mioyo yetu ili tujipatie maarifa katika hilo.

Luka 2:40, 52
Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.”
Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.”
Kupitia mistari hii unaweza kuona ya kwamba yule mtoto alipozaliwa hakukua ndani ya siku moja na kufa hapo hapo, bali alipitia hatua zote za ukuaji- naamini unaelewa ya kwamba ukuaji ni hatua, si mara moja (growth is gradual not sudden). Kadiri alivyoendelea kukua ndivyo alivyoukaribia mwisho wa maisha yake, lakini hakuwa anaishi kusubiri kifo. Kwa namna ya kawaida utagundua kwamba alikuwa anaishi kama vile hakuna kifo mbele yake, aliishi kwa kukamilisha kusudi la kuwepo kwake kabla ya kifo. Kitu ninachotaka uone hapa ni kwamba kuna kiasi cha muda (time gap) kati ya kuzaliwa na kufa au kwa maneno mengine kuna daraja linalounganisho hii miisho miwili ya maisha. Wacha nikuonyeshe kwa maneno rahisi kabisa… ni kwamba, wewe hukufa mara tu baada ya kuzaliwa (japo kuna matukio kama hayo) bali umeendelea kuishi mpaka leo ukielekea kifoni. Hicho ndiyo kipindi ninachopenda tukitazame mahala hapa.
                                                                      Yoeli 3:14                             
Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya BWANA i karibu, katika bonde la kukata maneno.”
Sote tunatambua wazi ya kwamba siku ya Bwana haitakuja kwenye ulimwengu wa maisha ya kabla ya kuzaliwa kwetu na twajua ya kwamba siku ya Bwana haitakuja kwenye ulimwengu ule wa maisha baada ya kifo. Siku ya Bwana inakuja kwenye ulimwengu huu wa maisha ya katikati ya kuzaliwa na kifo. Biblia inatufundisha ya kwamba Yesu hatakuja mara ya pili katika ulimwengu wa maisha baada ya kifo, bali atakuja kwenye ulimwengu huu na hata ndugu waliotangulia kuondoka kwa njia ya kifo na kuingia kwenye ulimwengu wa maisha baada ya kifo, nao watarejeshwa ili kuungana nasi kwenye huu ulimwengu (upande huu wa maisha) ndipo taratibu zingine zitafuata. (Ufunuo 1:7; 1 Thesalonike 4:13-17). Kwa lugha ya moja kwa moja ni kwamba bonde la kukata maneno ni kipindi kati ya kuzaliwa mpaka kifo, ni hilo jengo fulani ambalo mtu huingia kwa kuzaliwa na huondoka kwa kifo, yaani ni maisha mtu aishiyo baada ya kuzaliwa na kabla ya kufa. Ndugu msomaji, naomba uanze kusoma fundisho hili kwa kujitambua kwamba umo ndani ya bonde la kukata maneno!







Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP