Thursday, April 24, 2014

MAKUTANO YA TAI na JAMES KALEKWA

By Jimmy  |  9:04 AM No comments


PASAKA WA PILI NI UREJESHO WA KUSUDI KUU LA KWANZA LA UFALME WA MUNGU.

SEHEMU YA 2 


Nguvu na kwa msisitizo ni hili: Kilichomfanya Mungu aanze mpango wa kuwaokoa taifa lake teule si wingi wa maumivu yao, si ukubwa wa kilio chao, si masikitiko yao bali ni AGANO yaani mkataba/makubaliano aliyoyaweka na malango ya taifa la Israeli yaani Ibrahimu, Isaka na Yakobo (Israeli). Soma vizuri kwa umakini (Kutoka 2:23-25). Agano aliloliweka Mungu na taifa la Israeli lilianzia kwa baba wa mataifa yote Ibrahimu (Soma Mwanzo 22:15-19)
Kinachomvuta Mungu si kilio! Unaweza ukajiliza muda mwingi sana, halafu Mungu anakutazama tu kwasababu wingi wa machozi si chochote… Wakati mwingine Mungu anaamua tu kuchukuliana na sisi katika upumbavu na kutokujua kwetu, lakini kama “tai” unapaswa kujua ya kwamba Mungu hufanya kazi kwa kanuni na moja ya kanuni ni hii “Mungu hulitazama neno lake ili alitimilize”

Kwanini Mungu anataka Israeli watoke utumwani?


Kutoka 3:18
Ukisoma kwa jicho la kujifunza utagundua kuwa sababu kuu ya kutoka utumwani kwa wana wa Israeli ni kwenda kumtolea dhabihu Mungu wetu. Hicho ni kiashiria ya kwamba kwa kipindi chote cha utumwa na ufalme mwingine, wana wa Israeli hawakuwa wakimtolea Mungu dhabibu/sadaka.
Unaweza kujiuliza dhabihu/sadaka ni nini? Ina umuhimu gani kiasi hiki mpaka Mungu aamue kuanzisha harakati za uhuru wa taifa ili tu apate hicho kitu kinaitwa dhabihu?... Dhabihu ni ibada inayoonyesha hali ya mahusiano kati ya mtoaji na mpokeaji wa dhabihu. Pia ni njia aitumiayo mtoaji wa dhabihu kumtambua mpokeaji wa dhabihu kuwa ni mkuu katika maisha yake.
·         Ni shughuli ya kiroho (katika ulimwengu wa roho – si ulimwengu wa mwili)
·         Ni ibada ya kiushirika (fellowship)- mahusiano binafsi; mahusiano ya karibu (communion)
 
Wana wa Israeli walikosa kufanya tukio hili muhimu kwa kuwa walikuwa katika hali ya utumwa na chini ya ufalme.
Hivyo basi, Mungu anadai mahusiano na watu wake (taifa lake teule) na mahusiano hayo yanatakiwa kujengwa na kustawishwa katika mazingira huru (nje ya utumwa na ufalme wa Misri). Mungu angeweza kabisa kuomba dhabihu ilihali wana wa Israeli wakiwa Misri lakini hayo si mazingira sahihi ya kuyalea mahusiano yake na watu wake. Ni muhimu ukumbuke kuwa mazingira yaliyokuwako Misri yalikuwa ni:
·         Fikra za kitumwa (slavery mindset/mentality)
·         Miungu ya Misri
·         Ufalme wa Misri
·         Mabwana – wamiliki wa watumwa
Katika mazingira haya, hakuna uhusiano wa kudumu ungeweza kustawi.
  

Kutoka 12: 1-51
Baada ya Farao (mfalme wa Misri) kukataa kuwaachilia huru taifa teule la Mungu. Mungu anaandaa mpango usiozuilika wa ukombozi kwa njia ya sadaka/dhabihu iitwayo Pasaka. Wazo la jina la dhabihu/sadaka hii twalipata Kutoka 12:11… Ni Mungu mwenyewe ndiye aliyetoa maelekezo kwamba sadaka hiyo iitwe Pasaka, si fikra za Musa wala kiongozi awaye yote.
   
·         Mzaliwa wa kwanza
·         Asiye na mawaa
·         Asiye na ulemavu yaani mkamilifu
·         Wa kiume
Pia jambo jingine la msingi kutazama hapa ni kwamba, mwanakondoo huyo wa Pasaka hakuchinjwa hovyo hovyo tu, bali alichinjwa kimkakati (strategically). Ukisoma Kutoka 12:3-4 utabaini ya kwamba mwanakondoo alikuwa ni maalum kwaajili ya kuihifadhi nyumba fulani na kama watu wa nyumba walikuwa ni wachache basi walishirikiana na jirani zao… Maana yake ni kwamba mwanakondoo mmoja alikuwa ni kwaajili ya kufunika idadi ya watu kadhaa – Hii ni maalum sana.
nguvu na kwa msisitizo ni hili: Kilichomfanya Mungu aanze mpango wa kuwaokoa taifa lake teule si wingi wa maumivu yao, si ukubwa wa kilio chao, si masikitiko yao bali ni AGANO yaani mkataba/makubaliano aliyoyaweka na malango ya taifa la Israeli yaani Ibrahimu, Isaka na Yakobo (Israeli). Soma vizuri kwa umakini (Kutoka 2:23-25). Agano aliloliweka Mungu na taifa la Israeli lilianzia kwa baba wa mataifa yote Ibrahimu (Soma Mwanzo 22:15-19)
Kinachomvuta Mungu si kilio! Unaweza ukajiliza muda mwingi sana, halafu Mungu anakutazama tu kwasababu wingi wa machozi si chochote… Wakati mwingine Mungu anaamua tu kuchukuliana na sisi katika upumbavu na kutokujua kwetu, lakini kama “tai” unapaswa kujua ya kwamba Mungu hufanya kazi kwa kanuni na moja ya kanuni ni hii “Mungu hulitazama neno lake ili alitimilize”
  
Kutoka 3:18
Ukisoma kwa jicho la kujifunza utagundua kuwa sababu kuu ya kutoka utumwani kwa wana wa Israeli ni kwenda kumtolea dhabihu Mungu wetu. Hicho ni kiashiria ya kwamba kwa kipindi chote cha utumwa na ufalme mwingine, wana wa Israeli hawakuwa wakimtolea Mungu dhabibu/sadaka.
Unaweza kujiuliza dhabihu/sadaka ni nini? Ina umuhimu gani kiasi hiki mpaka Mungu aamue kuanzisha harakati za uhuru wa taifa ili tu apate hicho kitu kinaitwa dhabihu?... Dhabihu ni ibada inayoonyesha hali ya mahusiano kati ya mtoaji na mpokeaji wa dhabihu. Pia ni njia aitumiayo mtoaji wa dhabihu kumtambua mpokeaji wa dhabihu kuwa ni mkuu katika maisha yake.
·         Ni shughuli ya kiroho (katika ulimwengu wa roho – si ulimwengu wa mwili)
·         Ni ibada ya kiushirika (fellowship)- mahusiano binafsi; mahusiano ya karibu (communion)
Wana wa Israeli walikosa kufanya tukio hili muhimu kwa kuwa walikuwa katika hali ya utumwa na chini ya ufalme.
Hivyo basi, Mungu anadai mahusiano na watu wake (taifa lake teule) na mahusiano hayo yanatakiwa kujengwa na kustawishwa katika mazingira huru (nje ya utumwa na ufalme wa Misri). Mungu angeweza kabisa kuomba dhabihu ilihali wana wa Israeli wakiwa Misri lakini hayo si mazingira sahihi ya kuyalea mahusiano yake na watu wake. Ni muhimu ukumbuke kuwa mazingira yaliyokuwako Misri yalikuwa ni:
·         Fikra za kitumwa (slavery mindset/mentality)
·         Miungu ya Misri
·         Ufalme wa Misri
·         Mabwana – wamiliki wa watumwa
Katika mazingira haya, hakuna uhusiano wa kudumu ungeweza kustawi.

Pasaka wa kwanza ni nani/nini?

Kutoka 12: 1-51
Baada ya Farao (mfalme wa Misri) kukataa kuwaachilia huru taifa teule la Mungu. Mungu anaandaa mpango usiozuilika wa ukombozi kwa njia ya sadaka/dhabihu iitwayo Pasaka. Wazo la jina la dhabihu/sadaka hii twalipata Kutoka 12:11… Ni Mungu mwenyewe ndiye aliyetoa maelekezo kwamba sadaka hiyo iitwe Pasaka, si fikra za Musa wala kiongozi awaye yote.

Sifa ya dhabihu ya Pasaka (Kutoka 12:5):

Mzaliwa wa kwanza

·         Asiye na mawaa
·         Asiye na ulemavu yaani mkamilifu
·         Wa kiume
Pia jambo jingine la msingi kutazama hapa ni kwamba, mwanakondoo huyo wa Pasaka hakuchinjwa hovyo hovyo tu, bali alichinjwa kimkakati (strategically). Ukisoma Kutoka 12:3-4 utabaini ya kwamba mwanakondoo alikuwa ni maalum kwaajili ya kuihifadhi nyumba fulani na kama watu wa nyumba walikuwa ni wachache basi walishirikiana na jirani zao… Maana yake ni kwamba mwanakondoo mmoja alikuwa ni kwaajili ya kufunika idadi ya watu kadhaa – Hii ni maalum sana.

 

 


 

 













 


 





 

 







 




 




 

 




 

 







 



·       

 



Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP