Thursday, March 13, 2014

UNYESHA MOYO WA UPENDO MDAU WANGU TUWASAIDIE KITUO HIKI CHA WATOTO YATIMA.

By Jimmy  |  2:02 PM No comments



 Mwandaliwa islamic orphans home care and counselling support (mioca's) ni kituo cha kulelea watoto yatima, kituo hiki kilianzishwa mwaka 2002 chini ya uangalizi na usimamizi  wa mama Halima Ramadhani  Mpeta. kituo hiki kilifanikiwa kupata usajili wa namba 00NGO/1801 mwaka 2006, chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na Ofisi zake zipo mkoani Dar es salaam, Wilaya ya Kinondoni Kata ya Bunju, Mtaa wa mbweni, nyumba no. 02

Madhumuni ya uanzishwaji wa kituo hiki ni kulea watoto yatima waliopoteza wazazi wao na hivyo kupelekea watoto hawa kukosa Elimu, Malezi bora,  malazi, matibabu, na hata upendo. Hivyo kuweza kuwaepusha watoto hawa na majanga mabaya ya kidunia, kama uvutaji madawa ya kulevya, uasherati, n.k MIOCA imekua mstari wa mbele kuwasaidia  watoto hawa bila kujali dini, kabila, wala rangi.

Mpaka sasa kituo hiki kimefanikiwa kupata watoto wapatao 94, wa kiume ni 54 na wa kike ni 40, ambao ni wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi, sekondari, na chekechea. watoto wote hawa tunaishi nao hapahapa kituoni chini ya usimamamizi wa mama mlezi bi. halima.

Ndugu watanzania wenzetu tunapenda

kuwafahamisha juu ya changamoto zinazotukabili . kwa sasa kituo kinakabiliwa na deni la hospitali katika hospitali inayoitwa MICO RABININSIA MEMORIAL HOSPITALI Iliyopo Namanga Tegeta,  deni hili limetokana na matibabu ambayo watoto wamekuwa wakipata tangu february 2012 mpaka february 2014, tunadaiwa  kiasi cha tshs 7,797,900/=  msimamizi  wa hospitali anaomba kupatiwa pesa,  ili watoto waweze kuendelea kupatiwa tiba, tuna wakati mgumu katika kutimiza hili kwani ni uvumilivu mkubwa ambao ametuonyesha katika kuwasaidia watoto hawa hivyo tunawaomba ndugu wote mtakaosoma habari hii muweze kutuunga mkono. tuna imani kubwa sana kuwa ombi letu litapokelewa na kupatiwa ufumbuzi, kwa ushirikiano mtakaotupatia mtakuwa mmeweza kuwaokoa watoto hawa katika tatizo hili, kwani afya ni kitu muhimu katika maisha ya binadamu. ikizingatiwa watoto hawa hawana baba wala mama kwa hiyo wewe na yule mtakua ndio msaada pekee katika kuwaokoa watoto hawa.






 mwisho tunapenda kuwakaribisha sana katika kituo hiki, ili kwa pamoja muweze kuwasaidia watoto hawa. kama maneno ya mwenyezi mungu yanavyotufundisha kuwa "HUDUMA KWA MWANADAMU NI HUDUMA KWA MWENYEZI MUNGU." asanteni sana na karibuni MIOCA'S

kwa mawasiliano zaidi,

0715720022, 0759090290.
A/c no. ni 01j2080397900  Mioca'S, bank ya CRDB Tawi la mbezi beach.

 

Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP