Monday, March 24, 2014

HABARI ZIKUFIKIE MDAU WANGU,KWAYA YA UKOMBOZI KKKT MSASANI KUZINDUA RASMI AUDIO CD YAO "NAKUSHUKURU MUNGU"

By Jimmy  |  12:05 PM No comments


 Nakushukuru Mungu, Umenitoa Mbali kwenye shimo la dhambi, Sasa nafurahia ndani ya nyumba yako Baba Baba, sina cha kukulipa. Haya ni baadhi ya maneno yanayopatikana katika wimbo maarufu unaoitwa Nakushukuru Mungu ulioimbwa na Kwaya ya Vijana Msasani ambayo sasa inajulikana kama Kwaya ya Ukombozi.
Kwaya hii ya Ukombozi ni moja kati ya kwaya ambazo zimejipatia umaarufu mkubwa katika ramani ya muziki wa injili na kumtukuza Mungu ndani nan je ya mipaka ya Tanzania.
Kwaya hii pia iliwahi kusikika miaka ya mwishoni mwa 90 waliposhirikiana na muimbaji mkongwe Cosmas Chidumule katika album ya Kiatu cha Yesu ambapo kwaya hii ilishiriki kuitikia nyimbo zote pamoja na kupiga muziki katika album hii iliyotoa nyimbo maarufu kama Yesu ni Bwana na Libarikiwe Neno.
Ukombozi
ilianzishwa rasmi mwaka 1977 na ina makazi yake katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Msasani ikiwa na takribani waimbaji 50 ambao kwa pamoja wamenia kumtumikia Mungu kwa kutumia vipaji vyao vya muziki na uimbaji.

Mwaka jana mwanzoni kwaya ya Ukombozi iliingiza sokoni tena album ya video nyingine iitwayo Sabuni ya Roho ambapo ndani yake kulikuwa na wimbo maarufu uitwao Ni Kwa Neema na nyinginezo nyingi. Uzinduzi wa album hii ulishuhudiwa na wageni mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa aliyekuwa mgeni rasmi.
Mpaka sasa album ya Sabuni ya Roho imeshauza nakala takribani elfu tano na inazidi kufanya vizuri chini ya usambazaji wa kampuni ya Umoja Audio and Visual Company.
Kufuatia mafanikio haya kwaya hii inayofundishwa na walimu watatu imeamua kufanya ibada ya pekee ya kumshukuru Mungu siku ya tarehe 6 mwezi Aprili katika usharika wao wa nyumabani Msasani ambapo wageni mbalimbali wamealikwa kuhudhuria ibada hii.


Uzinduzi wa Nakushukuru Mungu Utakavyo kua.
Sadaka ya shukrani itakwenda sambamba na uzinduzi wa remix album ya Nakushukuru Mungu audio ambapo ndani yake kuna nyimbo kama Usinipite, Sema Kitu na Nakushukuru Mungu ambao umejizolea umaarufu miongoni mwa watanzania wengi.
Kwa mujibu wa mwenyekiti Bwana Mchome, Ukombozi walifikia maamuzi ya kuurudia wimbo huu ili uendane na teknolojia ya sasa maana watu wengi bado wanauhitaji na hivyo kwaya iliona ni vema kuitikia wito.
Kama ilivyo kwa album ya Sabuni ya Roho, Nakushukuru Mungu pia imefanyiwa kazi katika studio za CVC Chang’ombe chini ya mtayarishaji Steven Deffa ambaye ametengeneza album nyingi zinazofanya  vizuri kama Usiku wa Manane na Mtu wa Nne ya Kinondoni Revival Choir.
Hii ni siku ya muhimu kwao maana Biblia inasema  tumshukuru Mungu kwa kila jambo, hata kwa magumu tuliyopitia bado kumshukuru Mungu ni jambo muhimu sana
Siku hii pia itajumuisha mualiko wa waimbaji mbalimbali wa zamani waliombia kwaya hii ambapo wapo maaskofu kama Stephen Munga wa Dayosisi ya Lushoto na Profesa Godwill Mrema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao hawa wote waliwahi kuwa wenyeviti huko zamani.
Kwa mwaka huu kwaya imedhamiria kupanua mipaka ya kufanya huduma kwa kutembelea mikoa mbalimbali kumtangaza Kristo na pia iko katika mchakato wa kupata basi la kutumuia kwa ajili ya huduma yao.
 



Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP