Saturday, April 13, 2013

Friends On Friday Jubilation Hatari Caption ni saidie wewe....

By Jimmy  |  10:10 AM No comments

 
 Siku Ya Jana Katika Garden Ya Tamal Hotel Friends On Friday Kama Kawaida ilichukua mkondo wake, ambapo groups mbalimbali za Muziki wa Injili zilionesha Ustadi Mkubwa katika Live Performance.

Kikosi Kipya Cha Glorious Celebration kilionesha Makali yake kwa Vocal na "wese" juu yao na kuwashangaza wengi waliohudhuria katika Usiku wa Jana, Muonekano wao wa Sare uliwafanya kuonekana maridhawa kabisa.

Paul Clement mwanamuzi kutoka kundi la Glorious Worship Team kama ilivyo ada na kawaida alikwenda sawa kabisa nakuonesha ukongwe wake wa Muziki wa Injili katika muda mfupi aliokaa katika tasnia hii, nyimbo zake za kuabudu alioshusha uwepo mahali hapo usiku wa jana.

Felis Mubibya Mwanamuziki wa Kundi la Sowers ambaye anafanya muziki wa Injili nchini Marekani nae alikuwepo kwa ajili kunogesha shughuli nzima ya Friends On Friday. Akiongea na blog hii Felis alisema "muziki wa injili wa Tanzania unakuwa sana, tofauti na Marekani na Ulaya ambapo watu hucheza pia kwa kujificha ficha, lakini upigaji na arrangements za muziki wa live huleta radha kamili.

Wadau wakubwa wa Friends On Friday Miriam Lukindo wa Mauki na Steven Wambura walinogesha zaidi katika Event Ya Jana Usiku.


 Papaa akienda Sawa na 12 Disciples ndani ya Tamal

Kulia ni Furaha Masinga, Kati ni Edna Luvanda Kushoto ni Milembe wa Blogger Sasali.

Kitu Cha Ajabu zaidi zaidi Ya watu 10 usiku wa Jana wamejitolea ku-support Friends On Friday Kila Mwezi Kuhakikisha Inafanyika. Wamejitolea Kutoa Fedha zao, na wakati Huo Huo Tv Sibuka Kupitia Kipindi Chake Cha Gospel Hits na Clouds Tv Kupitia Kipindi Cha Chomoza wamejitolea Kuwa Wadhamini Wamojawapo wa Friends On Friday Kwa Mwaka 2013.

Tofauti na ilivyotarajiwa na watu kuona makundi hayo kama maadui, waliweza kushirikiana vyema viwanjani hapo ikiwa pamoja na kucheza pamoja walipoguswa, wapigaji wao kushirikiana kuwapigia waimbaji wengine na kukaa pamoja jambo ambalo watu wengi wamemtukuza Mungu kwa ajili ya makundi hayo.

 Mdau Mkubwa nambari wa FoF Shemeji Jacque Mndeme na mumewe aliye jificha na Camer.





 



 

 Mzee wa Saxerphone 


 









  











Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP