Monday, October 27, 2014

SABABU ZA ROSE KUCHIKICHIA FEDHA ZATOKANA NA UPASUAJI PAMOJA NA AFYA KUA MBAYA.

By Jimmy  |  9:53 AM No comments


Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum katikati ya wiki hii, Rose ambaye ameripotiwa kwa misala tofauti ya kuchikichia fedha za shoo hivi karibuni, amefunguka kuwa afya yake si nzuri kwani anasumbuliwa na mshipa kwenye mguu, akafanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Mkoa ya Dodoma.
“Siko vizuri kiafya nimefanyiwa upasuaji mguuni, nimeshonywa nyuzi nne lakini bado hali yangu si nzuri kiafya, nawaomba Watanzania waniombee,” alisema Rose kwa tabu na kuongeza:

“Hata ukiniona utanihurumia kwani mbali na upasuaji kwenye kidole gumba pia nimevimba sana uso.
“Kwa sasa nipo kitandani nyumbani kwangu najiuguza. Nitarudi tena hospitalini Jumanne ijayo.”
Akizidi kumwaga maneno kwa kinasa sauti cha Risasi Jumamosi, Rose alimshukuru mwandishi wa Barua Nzito iliyochapishwa katika gazeti tumbo moja na hili la Risasi Mchanganyiko (toleo lililopita) kwa kumuonya juu ya suala la kudaiwa kuingia mitini na fedha tofauti za shoo na kuomba radhi kwa Watanzania.

“Nawaomba sana radhi wote niliowakosea, niwaombe waniombee nipone na nitarejesha fedha zao,” alisema Rose.

Tunamuombea Rose kwa Mwenyezi Mungu ampe afya njema ili aendelee na huduma ya kumtumikia Mungu kwa njia ya nyimbo za Injili-Mhariri.
 Chazo:BaabKubwa

BaabKubwa



BaabKubwa


Jimmy Author: Jimmy

Hello, I am Author, decode to know more: In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. In commodo magna nisl, ac porta turpis blandit quis. Lorem ipsum dolor sit amet.

0 comments:

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By Bloggertheme9