i.Maisha baada ya kuzaliwa mpaka kifo
Japo
jamii nyingi huyatazama maisha ya mwanadamu katika hatua tatu: kuzaliwa, kuishi
na kufa na kimantiki inaweza kuonekana ni kweli lakini unapaswa kung’amua ya
kwamba kuzaliwa ni mlango wa kuingilia (entrance) na kifo ni mlango wa kutokea
(exit) kwenye jengo fulani. Katikati
ya hii miimo miwili ya kimaisha kuna wakati mkubwa wa maisha ambao ni vyema
tukaelekeza mioyo yetu ili tujipatie maarifa katika hilo.
