Showing posts with label James Temu news 11:39 Am. Show all posts
Showing posts with label James Temu news 11:39 Am. Show all posts

Thursday, June 12, 2014

MUENDELEZO WA MAISHA YA BAHATI BUKUKU





Japokuwa nimejitahidi sana kuisahau siku hii lakini moyo wangu umeshindwa kufanya hivyo. Kila ninapotulia, iwe sebuleni au chumbani kwangu, picha ya siku hiyo huwa inanijia kichwani mwangu. Tukio hilo limekuwa kubwa kwangu huku likiendelea kujirudia kama mkanda wa filamu.
Nilipenda kwenda shule kusoma, na hii ilikuwa njia mojawapo ya kuepuka kufanya kazi za nyumbani, hasa kuosha vyombo kitu nilichokuwa nikikichukia mno.
Japokuwa nilikuwa mtoto mdogo lakini mama alijitahidi sana kuniweka katika mazingira ambayo mtoto wa kike anatakiwa kuwa.
Achukia kuosha vyombo
Kila siku alikuwa akinitaka nioshe vyombo, hii ilikuwa kazi pekee niliyokuwa nikiichukia mno. Kila nilipokuwa nikirudi nyumbani, mama alikuwa akinipa maziwa na kiporo cha jana, nikimaliza kula, alikuwa akiniambia nioshe vyombo nilivyovitumia.
Nilikereka mno lakini sikuwa na jinsi, nilibaki nikilalamikalalamika lakini mwisho wa siku niliosha vyombo mbele yake huku akionekana kuwa na furaha.

E-mail Newsletter

Sign up now to receive breaking news and to hear what's new with us.

Recent Articles

© 2014 Uncle Jimmy | Distributed By My Blogger Themes | Created By BloggerTheme9
TOP